Kimataifa

Huzuni Mfalme Oyo wa Tooro nchini Uganda akifariki; chanzo bado hakijatajwa

Na REUTERS August 31st, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KAMPALA, Uganda:

MFALME Oyo Nyimba Kabamba Iguru Rukidi IV wa Tooro Uganda alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 34.

Waziri Mkuu wa ufalme huo, Calvin Armstrong Rwomiire Akiiki, alitangaza kifo chake Alhamisi usiku.

Mfalme huyo alifariki mwendo wa saa nne usiku, bila kilichosababisha mauti yake kusemwa hadharani.

Oyo alitwaa ufalme 1995 akiwa na umri wa miaka mitatu, baada ya kifo cha babake, Rukirabasaija Patrick David Matthew Kaboyo Olimi III, na kuwa mfalme mwenye umri mdogo zaidi duniani.

Uganda ni jamhuri inayoongozwa na rais aliyechaguliwa, lakini ina falme kadhaa za jadi ambazo zinaendelea kuwa na ushawishi mkubwa wa kitamaduni na kijamii, licha ya uwepo wa utawala wa urais.

Tooro iko magharibi mwa Uganda, karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Akiiki alisema mfalme huyo hakuwa ameoa, lakini aliacha mrithi na mwendelezo wa uzazi wake ambao umehakikishwa.

Kifo chake kimezua huzuni kubwa Uganda.

Kiongozi wa upinzani Bobi Wine alisema: “Habari za kusikitisha sana! Roho ya Mfalme ipumzike kwa amani ya milele.”