• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Mshukiwa wa ugaidi kusalia ndani hadi kesi iamuliwe

Mshukiwa wa ugaidi kusalia ndani hadi kesi iamuliwe

Ahmed Yusuf Okoth katika mahakama ya Nairobi aliponyimwa dhamana kwa kosa la ugaidi. Picha/Richard Munguti

RICHARD MUNGUTI

MSHUKIWA wa ugaidi, Ahmed Yusuf Jumatatu aliamriwa akae rumande kwa kosa la ugaidi hadi kesi inayomkabili isikizwe na kuamuliwa.

Hakimu mkuu Francis Andayi  alikataa ombi la mshtakiwa la kuachiliwa kwa dhamana akisema, “atachana mbuga akiachiliwa huru kwa sasa.”

Bw Andayi alisema adhabu ya kosa linalomkabili mshtakiwa ni kali  kwa vile ni kifungu cha miaka 30 kwa kosa la kushiriki katika ugaidi.

Anakabiliwa na mashtaka matano miongoni mwao kutoa mafunzo ya ugaidi kwa wanafunzi wa shule eneo la Trans-Nzoia.

Akisoma uamuzi alisema , “Upande wa mashtaka umethibitisha kwamba utatoroka ukipewa dhamana.”

Mshtakiwa atakaa rumande hadi kesi iamuliwe. Ushahidi utaanza kutolewa Machi 16.

You can share this post!

Hakimu aamuru anayedaiwa kuiba kioo apelekwe hospitalini...

Hata mruke angani, marufuku ya makaa itadumu, aapa Gavana...

adminleo