• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Nairobi yatajwa jiji bora la mikutano ya kibiashara Afrika

Nairobi yatajwa jiji bora la mikutano ya kibiashara Afrika

NA LEONARD ONYANGO

JIJI la Nairobi kwa mara nyingine limeibuka bora zaidi kwa safari za kibiashara barani Afrika katika Tuzo za Safari Duniani (WTA).

Katika makala hayo ya 26 ya tuzo za WTA yaliyofanyika Mauritius, Jumba la Kimataifa la Jomo Kenyatta (KICC) pia liliibuka bora kwa kuwa na kumbi murua za mikutano na makongamano barani Afrika.

“Tumefurahi sana kutuzwa kwa kuibuka bora Afrika. Tuzo hizo zimethibitisha kuwa kweli Nairobi na jumba la KICC ni bora zaidi barani,” akasema Mkurugenzi Mtendaji wa KICC Nana Gecaga aliyekuwa akizungumza alipopokezwa tuzo hizo.

“Tuzo hizo zitasaidia pakubwa katika kuinua sekta ya utalii humu nchini,” akaongezea.

Jumba la KICC lilibwaga majumba mengine barani Afrika kama vile ukumbi wa mikutano wa Cairo (Misri), Cape Town Convention Centre nchini Afrika Kusini, Durban Convention Centre (Afrika Kusini), Kigali Convention Centre (Rwanda), Palais Des Congress Marrakech (Morocco) na Sandton Convention Centre (Afrika Kusini).

Hii ni mara ya kwanza KICC kushiriki katika tuzo hizo na kulipiku jumba la Durban ambalo limeshinda tuzo kwa mara ya tisa.

You can share this post!

Hofu mahindi yataisha Kenya majuma 3 yajayo

Tahadhari mvua kubwa itanyesha kote nchini kwa wiki nzima

adminleo