• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Kenya yang’aa kwenye tenisi U-12

Kenya yang’aa kwenye tenisi U-12

Na GEOFFREY ANENE

WANATENISI wa Kenya waling’aa katika mashindano ya Afrika Mashariki ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 12 yaliyokamilika Februari 8, 2018 jijini Kigali.

Wenyeji Rwanda walitwaa taji la wasichana wakifuatwa na Wakenya, Burundi na Uganda katika usanjari huo. Rwanda pia iliibuka mshindi katika kitengo cha wavulana ikifuatiwa na Burundi, Kenya na Uganda, mtawalia.

Katika siku ya mwisho, Kenya ilipepeta Burundi kwa mechi 3-0 katika kitengo cha wasichana na kulaza Uganda kwa mechi 2-1 katika kitengo cha wavulana.

Kwenye kitengo cha wasichana cha mchezaji mmoja mmoja, Anouk Vandevelde alimlima Zaituni Akesa 6-0, 6-0 naye Reha Kipsang’ akamshinda Milka Nkeshima japo kwa jasho 6-4, 6-4. Ushirikiano wa Vandevelde na Kipsang’ uliwabwaga Akesa, ambaye alishirikiana na Kinzey Umuvyeyi, 6-2, 6-0.

Kwenye kitengo cha wavulana, Liberty Kibue alilemea Allan Otto 6-1, 6-0 naye Raqeem Virani akapigwa 6-1, 6-4 na Troy Zziwa. Ushirikiano wa Kibue na Virani ulifanikiwa kuchapa Brian Kimera na Zziwa 7-5, 6-0 katika kitengo cha wachezaji wawili wawili na kushinda Waganda hao kwa mechi 2-1.

Rwanda pia ilikuwa na siku nzuri Alhamisi ilipopepeta Uganda 3-0 (wasichana) na Burundi 2-1 (wavulana).

Mashindano haya yaliyovutia Kenya, Rwanda, Burundi na Uganda, yalianza Machi 4 na kukamilika Machi 8.

You can share this post!

Wanyama ashinda tuzo ya goli bora la Februari EPL

Starlets kutoana jasho na She-polopolo ya Zambia

adminleo