• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Wanyama na Mariga kucheza pamoja Stars ikilimana na Comoros, CAR

Wanyama na Mariga kucheza pamoja Stars ikilimana na Comoros, CAR

Na GEOFFREY ANENE

KOCHA Stanley Okumbi ametaja kaka ya nyota wa Tottenham Hotspur Victor Wanyama, McDonald Mariga, katika kikosi chake kitakachopimana nguvu dhidi ya Comoros na Jamhuri ya Afrika ya Kati nchini Morocco mwezi Machi 2018.

Mara ya mwisho kiungo Mariga, 30, ambaye anasakata soka yake ya malipo katika klabu ya Real Oviedo inayoshiriki Ligi ya Daraja ya Pili ya Uhispania, alichezea Stars ni Machi 26 mwaka 2011 dhidi ya Angola.

Mbali na Mariga, Okumbi pia amerejesha kikosini Ismael Gonzalez, ambaye alichezea Stars mara ya mwisho mwaka 2016. Mzawa huyu wa Uhispania anasakata soka katika klabu ya Fuenlabrada inayosiriki Ligi ya Daraja ya Tatu nchini Uhispania.

Vilevile, Paul Were (Kaisar, Kazakhstan), Eric Johana Omondi (Brommapojkarna, Uswidi), Ayub Timbe (Heilongjiang FC, Uchina) na Francis Kahata (Gor Mahia) wamerejea kikosini baada ya kukwekwa pembeni kwa muda mrefu.

Hata Wanyama, ambaye ameshinda taji la goli bora kwenye Ligi Kuu ya Uingereza mwezi Februari, pia amekuwa nje muda mrefu. Alikuwa na jeraha baya mwisho wa mwezi Agosti mwaka 2017 lililomweka mkekani hadi mapema Januari mwaka 2018.

Mvamizi Michael Olunga, ambaye ni Mkenya wa kwanza kufunga mabao matatu kwenye mechi moja ya Ligi Kuu ya Uhispania na winga matata Ayub Timbe pia wamo kikosini.

Sura mpya kikosini ni Erick Kapaito ambaye amekuwa akifanya vyema kwenye Ligi Kuu ya Kenya msimu huu wa 2018.

Baadhi ya majina makubwa ambayo yamekosa namba ni mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Kenya mwaka 2017 Masoud Juma (Cape Town City FC, Afrika Kusini) na mwanasoka bora wa Kenya mwaka 2017, Michael Madoya (Zoo Kericho).

Juma amekuwa akiuguza jeraha naye Madoya bado hajaridhisha Okumbi. Timu itaanza mazoezi Machi 19. Mechi ya Comoros ni Machi 24 nayo ya Jamhuri ya Afrika ya Kati ni Machi 27. Zote zitapigiwa mjini Marrakech.

Kikosi cha Harambee Stars:

Makipa

Patrick Matasi (Posta Rangers), John Oyemba (Kariobangi Sharks), Faruk Shikalo (Bandari)

Mabeki

Harun Shakava (Gor Mahia), Brian Mandela (Maritzburg United, Afrika Kusini), David Ochieng, (Brommapojkarna, Uswidi), David Owino (Zesco, Zambia), Abud Omar (Slava Sofia, Bulgaria)

Viungo

Patilah Omoto (Kariobangi Sharks), Francis Kahata (Gor Mahia), Duncan Otieno (AFC Leopards), Samuel Onyango (Gor Mahia), Athuman Ismael Gonzales (Fuenlabrada, Uhispania), Anthony Akumu (Zesco, Zambia), Victor Wanyama (Tottenham Hotspurs, Uingereza), McDonald Mariga (Real Oviedo, Uhispania), Johanna Omollo (Cercle Brugge, Ubelgiji), Paul Were (Kaisar, Kazakhstan), Eric Johana Omondi (Brommapojkarna, Uswidi)

Washambuliaji

Ayub Timbe (Heilongjiang FC, Uchina), Cliffton Miheso (Buildcon FC, Zambia), Erick Kapaito (Kariobangi Sharks), Jesse Were (Zesco FC, Zambia), Michael Olunga (Girona FC, Uhispania)

You can share this post!

Starlets kutoana jasho na She-polopolo ya Zambia

Kenya U-23 kuchuana na Uzbekistan Machi 22

adminleo