• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Mwanamume ashtaki korti kwa kumfanyia upasuaji wa ‘kujifungua’

Mwanamume ashtaki korti kwa kumfanyia upasuaji wa ‘kujifungua’

MASHIRIKA Na PETER MBURU

MWANAMUME wa miaka 34 kutoka Louisville ameshtaki hospitali moja baada ya kumfanyia upasuaji unaofanyiwa wanawake wenye matatizo ya kujifungua, madaktari wakidhani kuwa alikuwa mjamzito.

Leslie Morgan White, mwanamume wa umbo nene ambaye ana historia ya kuvamiwa na ugonjwa wa moyo anadaiwa kuwa alipiga simu kwa 911 baada ya kuugua, alipohisi maumivu kifuani.

Alipelekwa katika hospitali ya St Mathews, ambapo punde tu madaktari walipomwona walimkimbiza katika mahali pa kina mama kujifungua, na wakamdunga dawa za kumlaza.

Kulingana na rekodi za matibabu, madaktari walianza kumfanyia upasuaji lakini wakabaini kuwa hakuwa mja mzito, wala tumbo la mtoto.

“Nilikuwa nikilia, nilikuwa nikihisi uchungu ndipo wakaniuliza ikiwa nilihitaji kudungwa dawa za kulazwa na nikakubali. Nashangaa kwani hakuna aliyeona uume wangu?” akashangaa White.

Alidai kuwa iliwachukua madaktari nusu saa baada ya kumfanyia operesheni hiyo ndipo wakagundua tatizo lake na wakaanza kumtibu kifua na moyo.

You can share this post!

Wakenya hutumia WhatsApp, Facebook sana usiku –...

Kiir apiga marufuku uimbaji wimbo wa taifa wakati hayuko

adminleo