• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 1:15 PM
Kenya kutuma ombi kuandaa kongamano la UN kuhusu utalii wa kimataifa

Kenya kutuma ombi kuandaa kongamano la UN kuhusu utalii wa kimataifa

Na MAGDALENE WANJA

KENYA ni miongoni mwa nchi ambazo zimeonyesha nia ya kuwa mwenyeji wa kongamano la baraza la Umoja wa Mataifa kuhusu Utalii wa Kimataifa ambalo litafanyika mwaka wa 2021.

Kulingana na Waziri wa Utalii Najib Balala, Kenya itawasilisha maombi yake rasmi wiki hii.

Waziri Balala alisema kuwa nchi ya Kenya imeonyesha ukomavu katika kuandaa hafla za kimataifa na hii inaiweka katika nafasi nzuri ya kuandaa mkutano huo.

Mataifa mengine yaliyoonyesha nia hiyo ni Morocco na Ufilipino.

“Tutawasilisha ombi letu la kuandaa kongamano hilo na tutakuwa nchi ya kwanza ya Afrika Mashariki kuandaa mkutano huo iwapo azma yetu itafua dafu,” alisema Bw Balala.

Ikifaulu, nchi hii bila shaka itapata faida kubwa kutokana na biashara za kigeni kwani idadi kubwa ya watalii wanatarajiwa kuzuru kipindi hicho.

“Hii itakuwa hatua kubwa katika kufungua njia kwa nchi ya Kenya kuandaa mikutano ya haiba kama hii siku zijazo,” akasema waziri.

You can share this post!

WAWERU: Aibu mabilioni kuporwa huku kukishuhudiwa uhaba...

Wakazi wa Makongeni kufurahia huduma bora za usafiri baada...

adminleo