• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
MAWAIDHA YA KIISLAMU: Dhana mbaya ina uwezo wa kuua udugu baina ya watu, na ni hatia

MAWAIDHA YA KIISLAMU: Dhana mbaya ina uwezo wa kuua udugu baina ya watu, na ni hatia

Na HAWA ALI

SIFA zote njema anastahiki Mwenyezi Mungu Subuhaanahu Wa Ta’ala, rehema na Amani zimshukie kiongozi wa umaah, Mtume wetu Muhammad, Swallallahu ‘alayhi Wasallam, maswahaba wake watukufu na watangu wema hadi siku ya Qiyaamah.

Uislamu umehimiza sana kutilia nguvu mafungamano ya mapenzi baina ya Waislamu na kuimarisha kamba ya udugu baina ya Waumini. Mtume Swallallahu ‘alayhi Wasallam akaita watu kwenye kila lenye kutilia nguvu mapenzi kama vile kutoa salamu, kupeana mikono wakati wa kukutana na mengineyo. Na ameonya kila lenye kudhoofisha mapenzi haya, kama vile kudhaniana vibaya, kusengenya, kufitini na yasiyokuwa hayo. Dhana mbaya ni njia pesi ya kueneza uadui, chuki, kukatana familia kutengana na kuvunja undugu wa Kiislamu.

Miongoni mwa maafa yaliyowasibu watu na jamii ni dhana mbaya, jambo ambalo linakata mapenzi kati ya watu, na mwenye dhana mbaya huwaangalia watu kwa jicho ovu, na bila shaka dhana mbaya ni kinyume na sheria ya Kiislamu.

Ili mafungamano baina yetu na watu yabaki imara ni kuwakabili watu hali ya kuwa nyoyo zetu zimesalimika pia kuwa safi na nyuso kuwa na bashasha na kuwadhania watu kwa dhana nzuri pindi tunaposalimiana nao.

Tunapozingatia mafungamano ya Waislamu yamesambaratika kutokana na dhana mbaya. Unaposikia maongozi ya Waislamu tunasikia wakisema fulani amekusudia hivi, na fulani ametaka jamabo hili. Yote yanapelekea kupatikana kwa chuki na mwisho ni kuvunjika au kusambaratika kwa mafungamano.

Dhana mbaya inapeleka kufuatilia aibu za watu na kuchunguzana kwa ajili hiyo utasikia kwa mwenye dhana mbaya akisema ‘Nitajaribu kuhakikisha’ basi atachunguza na kusengenya na kumtaja mwenzake kwa uovu.

Kuenea kwa dhana mbaya kunakosekana uaminifu kati ya watu na kukatana jambo ambalo kwamba linapelekea kutofaulu katika mambo yetu.Anasema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala): Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake wala msizozane, msije mkaharibikiwa na kupotea nguvu

Tazama watu waovu walivyo wakejeli Waislamu na kuwadhania maovu pindi Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala) Aliposema: Kisha wale wabaya watasema: Imekuwaje, Mbona hatuwaoni wale watu tulikuwa tukiwahesabu katika waovu kwa kumfuata Muhammad. Je, tuliwafanyia mzaha (huko duniani, na hali yakuwa ni watu wakubwa Akhera au wamo Motoni humu pamoja na sisi) ila macho yetu hayawaoni tu?

Anasema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala): Enyi mlioamini, Jiepusheni sana na dhana mbaya. Kwani dhana mbaya ni dhambi.

Inajulisha Aya katika kuhifadhi heshima ya Muislamu kwa kutangulia na katazo la dhana. Ni uzuri ulioje kwa mujtama ulio salimika na dhana mbaya. Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) amesema: [Jiepusheni na dhana hakika ya dhana ni maongezi ya uongo wala msichunguzane wala msichukiane kuweni ndugu katika waja wa Mwenyezi Mungu].

Wamesema baadhi ya wanavyuoni dhana ambayo inafaa kuepukwa ni ile ambayo kwamba haijulikani njia yake kuwa ni ya sawa na sababu iliyokuwa ya wazi, mfano anayedhaniwa akiwa ni mtu mwema na akapewa amana kuwadhania kuwa amefanya khiana ni haramu. Kinyume na ambaye anajulikana anafanya maovu wazi wazi kwa ajili hiyo wamesema wanavyuoni dhana mbaya kwa mtu mwema haifai na hapana tatizo kudhania uovu mtu muovu.

Imepokewa hadithi Said ibn Musaib akisema: “Amewaandikia baadhi ya maswahaba kutowacha kufanya wema kwa jambo la ndugu yake maadamu hujashindwa wala asidhani neno baya limetoka kwa ndugu yako ikiwa inawezekana kuchukulia kwa uzuri na huo ndio mfano wa watu wema pindi wanaposhindwa kuelewa baadhi ya maneno, kwa kuwahukumu makosa watu wengine bila ya kuzingatia nia na hali ya yule mtu”.

Ibn Qayyim amesema: “Neno moja husemwa na watu wawili mmoja wao anakusudia haki na mwingine wao anakusudia batili kwa ajili hiyo hahukumiwi mtu kuwa kafiri kwa aliyesema “Ewe Mola wangu wewe ni mja wangu na mimi ni mola wako” hakukusudia kujifanya Mwenyezi Mungu. Amesema Sheikhul Islam Ibn Taymiyya pindi anaponukuu maneno ya wenye kumkhalifu akisema “Maneno haya yana upana, na haki huchukuliwa kwa uzuri na batili huwa na mambo mengi”

Mwanadamu hana haki kwa ndugu yake isipokuwa kwa mambo yaliyo wazi. Amepokea Abdulrazaq kutoka kwa ‘Umar Ibn Khattab akisema: “Watu walikuwa wakipokea wahyi wakati wa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) na wahyi ukakatika, lakini tunachukua sasa kwa yale yaliyodhihiri kutokana na vitendo vyenu kwa atakae dhihiri kheri tutamuamini na tutamkaribisha haitujalishi sisi usiri wake na Mwenyezi Mungu ndiye atakayemhesabu kutokana na usiri wake na atakae dhihiri shari lake kwetu hatutomuamini wala hatutomsadiki hata akisema kuwa usiri wake ni mwema”.

You can share this post!

CARABAO: Arsenal, Chelsea kulimana na Liverpool na...

MBURU: Mswada ukifaulu utazima hospitali kuzuilia wagonjwa,...

adminleo