• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
MAPISHI NA UOKAJI: Jinsi ya kuoka kuku kwenye ovena

MAPISHI NA UOKAJI: Jinsi ya kuoka kuku kwenye ovena

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa mapishi: Saa 1

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • kuku 1 (usikate vipande)
  • siagi kikombe ½
  • chumvi
  • pilipili manga
  • thyme
  • majani ya rosemary
  • foil paper
  • curry powder
  • majani ya giligilani
  • juisi ya limau
Kuku safi kabla kuokwa. Picha/ Margaret Maina

Maelekezo

Washa ovena na acha ipate joto hadi nyuzi 325.

Weka kuku safi kwenye sinia ya kuokea au chombo chochote cha kutumika wakati wa kuoka na kinachoingia kwenye ovena.

Paka siagi juu ya kuku hadi ienee vizuri.

Paka curry powder kwa ndani ya kuku. Curry ni mchanganganyiko wa viungo vingi tofauti, hivyo ni mahsusi kuleta ladha tamu na harufu nzuri itakayofanya chakula kinukie vizuri.

Nyunyizia chumvi kisha sambaza kwa ndani na nje vizuri.

Paka pilipili manga ya kutosha juu ya kuku.

Nyunyizia juisi ya limaou ya kutosha, kisha weka majani yaliyosagwa ya thyme na rosemary.

Funga nyama ya kuku kwenye foil paper kisha weka kwenye ovena.

Oka kuku wako kwa muda wa saa moja. Huu ni muda mzuri kwa kuku kuiva vizuri nje na ndani.

Baada ya muda kuisha angalia kama nyama ya kuku imeiva vizuri.

Nyama hii ikiiva, itoe kwenye ovena. Weka pembeni ili ipoe kisha pakua, katakata na ufurahie.

You can share this post!

ULIMBWENDE: Epuka makosa haya wakati wa kuosha nywele zako

MKASA: Wabunge waliweka lawamani shirika la huduma za feri

adminleo