• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Wahalifu wawaua maafisa wawili wa polisi Kayole

Wahalifu wawaua maafisa wawili wa polisi Kayole

Na VINCENT ACHUKA

MAAFISA wawili wa polisi waliokuwa wanapiga doria wameuawa kwa kupigwa risasi katika hali tatanishi Ijumaa asubuhi, Kayole, Nairobi.

Mamlaka zinasema maafisa hao wawili wa cheo cha konstebo na ambao walikuwa wa kituo cha polisi cha Obama walikuwa wanashika doria eneo la Mwenyenge walipovamiwa na wahalifu na kuuawa karibu na daraja la Saika Kayole.

Uhalifu huo ulitekelezwa saa kumi za asubihi.

“Afisa mmoja wa polisi amepigwa risasi kifuani huku mwingine akimiminiwa risasi kichwani,” polisi imesema.

Maganda matano ya risasi zilizotumika yalipatikana katika eneo hilo.

Wahalifu hao wameibwa bunduki za maafisa na simu zao.

You can share this post!

Hali ngumu wanayopitia baadhi ya wauzaji wa nguo

WANDERI: Afrika itahadhari kuhusu nia halisi ya Urusi

adminleo