• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 3:25 PM
Polisi azuiliwa kwa kupoteza bunduki

Polisi azuiliwa kwa kupoteza bunduki

Na Dickens Wasonga

POLISI mmoja anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Siaya baada ya kupoteza bunduki yake.Kulingana na Kamanda wa Polisi katika kaunti hiyo Bw Francis Kooli, haikubainika hali iliyomfanya polisi huyo kupoteza bunduki hiyo.

Kundi maalum la polisi tayari limebuniwa ili kuchunguza suala hilo.

Duru ziliiambia ‘Taifa Leo’ kwamba polisi huyo alishambuliwa na watu wawili waliokuwa wakisafiri kwa pikipiki, ambapo wanaaminika kupotea na bunduki hiyo baada ya kumnyang’anya.

Duru zilieleza kuwa polisi huyo alikumbana na kisa hicho mwendo wa saa tatu usiku mnamo Jumanne alipokuwa akielekea kituoni. Alikuwa akilinda afisi ya kamishna wa kaunti.

“Tunachunguza ikiwa polisi huyo alikuwa peke yake na ikiwa alikuwa kazini. Kwa kawaida, polisi walio kazini huwa wawili wawili. Hayo ni mambo makuu tutakayozingatia tutakapokuwa tukiendesha uchunguzi wetu,” akasema Bw Kooli.

You can share this post!

PRESHA URENO: Ronaldo na wenzake kikosini wanalenga...

Wabunge wa Pwani waomba waathiriwa wa mafuriko wasaidiwe

adminleo