• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 9:55 AM
SIHA NA ULIMBWENDE: Manufaa ya kutumia mafuta ya ‘Bio-Oil’ mwilini

SIHA NA ULIMBWENDE: Manufaa ya kutumia mafuta ya ‘Bio-Oil’ mwilini

Na MARGARET MAINA

[email protected]

BIO-Oil ni mafuta yanayosifika sana na wengi hupenda kuyatumia.

Kuondoa michirizi

Moja kati ya matumizi makubwa sana ya Bio-Oil ni kuondolea michirizi. Michirizi ni mistari inayotokea kwenye ngozi sanasana tumboni na mapajani kutokana na ngozi kupoteza uwezo wake wa kuvutika. Matumizi ya Bio-Oil kwa usahihi husaidia kupunguza ama kuondoa kabisa tatizo la michirizi katika ngozi.

Kuondoa makovu

Bio-Oil husaidia sana kuondoa makovu, hasa mtu anapoanza kutumia mapema mara tu baada ya kidonda au jeraha kupona.

Makovu machanga hupona haraka zaidi kuliko makovu ya muda mrefu.

Kutibu ngozi iliyosinyaa na kunyauka

Kwa mtu mwenye ngozi iliyoanza kuzeeka au iliyozeeka, basi atumie Bio-Oil. Baada ya muda, ngozi yake itarejea hali ya uzuri na yenye afya.

Kutibu ngozi kavu/ Ngozi iliyokauka

Bio-Oil inasaidia kuboresha afya ya ngozi na kuiwezesha iwe na maji na unyevu wa kutosha. Ngozi kavu ni rahisi kuzeeka na kwa hiyo matumizi ya Bio-Oil yatasaidia kuzuia ngozi kuzeeka kwa urahisi.

Kurekebisha rangi tofauti za ngozi na kuifanya iwe rangi moja

Bio-Oil husaidia kurejesha afya ya seli za ngozi na kusaidia mwonekano wake mzuri.

Husaidia kuondoa rangi mbaya zisizopendeza zinazotokana na athari za jua, vipodozi, kuungua na kadhalika.

Matokeo yake ni kuwa na ngozi nzuri yenye kupendeza na rangi inayofanana.

Bio-Oil hupatikana kwenye maduka ya dawa na maduka ya vipodozi.

You can share this post!

SIHA NA ULIMBWENDE: Jinsi ya kutumia juisi ya karoti...

Shughuli za usafiri zarejelewa kama kawaida Lamu siku moja...

adminleo