• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:38 AM
Tetesi kasisi alitumia ndumba kupora mke

Tetesi kasisi alitumia ndumba kupora mke

Na CORNELIUS MUTISYA

NZAIKONI, MACHAKOS

Pasta mmoja wa eneo hili ameingiwa na kibaridi baada ya tetesi kutanda mtaani kuwa alitumia nguvu za giza kumzamisha mume wa muumini wake aliyekuwa hasimu wake mkuu ili amchukue mkewe!

Kulingana na mpambe wetu, pasta huyo alikuwa akishukiwa kuwa na uhusiano wa kimahaba na mke wa jamaa huyo.

Tetesi hizo zilitanda mitaani mithili ya cheche za moto nyikani na zikamkera mno kalameni huyo.

“Uvumi kuwa pasta alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa polo huyo zilimchongea. Uadui ulizuka baina ya mtumishi wa Mungu na mume wa mwanamke huyo,’’ alieleza mdaku wetu.

Inasemekana kwamba, ili kulipiza kisasi, mume wa mwanamke huyo aliyekuwa ameteuliwa kiongozi wa wanawake kanisani humo alianza kuambia watu eti pasta huyo alikuwa Mfarishayo aliyekuwa akihubiri maji na kubugia mvinyo!

“Alieleza watu kwamba pasta alikuwa mzinifu mkuu na kwamba alitumia wadhifa wake kuvuruga boma za watu.

Aliapa kumkomesha pasta huyo kwa mbinu ambazo hakueleza watu,” alisema mdokezi.

Uhasama wa polo na pasta ulizidi na kufikia kilele walipokutana kisadfa njiani na polo akamchapa akimlaumu kwa kumnyemelea mkewe.

Hata hivyo, pasta alimuambia polo ya kwamba baada ya muda wa wiki mbili, angekiona cha mtema kuni.

“Vitisho vya pasta huyo vilitimia kikamilifu wakati polo huyo alipoanza kudhoofika mwili na kutatizika akili,’’ alisema mdaku wetu.
Wakazi walidai alimroga jamaa huyo ili amnyakue mkewe.

Kwa sasa, pasta huyo anaogopewa mno eneo hili na hakuna mtu yeyote anayethubutu kumchezea wengi wakimtaja kama “moto wa kuotea mbali.”

…WAZO BONZO 1…
…WAZO BONZO 2…
…WAZO BONZO 3…

You can share this post!

Makamishna wamtoroka Chebukati wakisema ameshindwa na kazi

Onyo kwa wanaouza dawa za hospitali za umma

adminleo