• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Taabani kwa kugeuza kondoo wa babake mke na ‘kurina asali’ mara saba

Taabani kwa kugeuza kondoo wa babake mke na ‘kurina asali’ mara saba

Na TITUS OMINDE

MWANAMUME wa umri wa miaka 30 alifikishwa katika mahakama moja mjini Eldoret kujibu mashtaka ya kushiriki ngono na kondoo wa babake.

Mlalamishi Sang Kibii ambaye ni baba wa mshtakiwa alisababisha kicheko kortini alipodai kuwa mwanawe amekuwa akishiriki tendo hilo na kondoo wake kwa zaidi ya mara saba.

Maelezo ya mashtaka yalisema kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo Aprili 13 mwaka huu kaitka eneo la Chepkanga viungani mwa mji wa Eldoret.

Mshtakiwa William Kipchirchir Kibii ambaye alikana mashtaka hayo mbele ya hakimu mkuu wa Elodret Bw Charles Obulutsa, alionekana kujikanganya pale alipokiri kuwa amewahi kushiriki ngono na kondoo huyo mara moja wala si mara mbili kama ilivyodaiwa.

Juhudi za mahakama kushawishi pande mbili husika kutafuta suluhu nje ya mahakama ziligonga mwamba kwani babake mshtakiwa aliambia mahakama kuwa tabia ya mwanawe ilikuwa imezidi ambapo alitaka apate funzo kupitia kwa sheria.

“Mheshimiwa nimechoshwa na kijana wangu ameshindwa kutafuta mke badala yake amebadilisha kondoo wangu kuwa mke wake,” aliambia mahakama  mzee mwenye ghadhabu.

Mahakama iliamuru mshtakiwa kuachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu ya Sh10,000, kesi hiyo itasikizwa Aprili 25 mwaka huu.

You can share this post!

Shinikizo kumtaka Chebukati pia ajiuzulu

Wabunge wa Kenya waduwazwa 3-1 na wenzao wa Uturuki

adminleo