• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 8:50 AM
Matrilioni ya pesa sasa hutumwa kwa simu

Matrilioni ya pesa sasa hutumwa kwa simu

Na BERNARDINE MUTANU

Takwimu kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini ilionyesha kuwa katika robo ya 2017 kufikia Septemba 30, mapato yalikuwa ni 714.3 bilioni.

Lakini katika robo ya Desemba, kiwango hicho kilishuka hadi Sh308.6 milioni ikilinganishwa na Sh352.4 milioni katika robo ya Septemba.

Idadi ya  waliotuma pesa kwa kutumia simu ilikuwa ni watu milioni 30 na maajenti walikuwa ni 198,234 katika kipindi hicho.

Lilikuwa ongezeko kutoka watu 28.1 milioni na maajenti 184,537 muda huo mwaka uliotangulia.

Kwa jumla kulikuwa na mashirika na watu walituma au kupokea pesa mara 607.4 katika kipindi hicho, biashara ya thamani ya Sh1.763 trilioni.

M-Pesa ndio ilikuwa na biashara iliyonoga zaidi kwa kutuma ua kupokea pesa mara 493 milioni, za thamani ya Sh1.4 trilioni na kufuatwa na Equitel(Benki ya Equity) ambayo ilitumiwa mara milioni 110, kwa thamani ya Sh306 milioni katika kipindi hicho.

You can share this post!

Vivukio 11 kujengwa kwenye barabara ya Outering

ERC kuwakamata wanaouza mafuta yanayoharibu injini za magari

adminleo