• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
SENSA: Simu nyingi nchini zinamilikiwa na wanawake

SENSA: Simu nyingi nchini zinamilikiwa na wanawake

Na DIANA MUTHEU

WANAWAKE wengi nchini Kenya wana simu za mkono kuliko wanaume, ripoti iliyoandaliwa na Shirika la Takwimu Nchini (KNBS), imeonyesha.

Kulingana na ripoti hio ya Sensa iliyotolewa Ijumaa wiki jana, kwa jumla, idadi ya watu wanaomiliki simu za rununu nchini ni 20.6 milioni.

“Watu hawa ni kutoka umri wa miaka mitatu na zaidi,” ikasema ripoti.

Hata hivyo, ripoti ilithibitisha kuwa idadi ya wanawake wanaomiliki rununu iko juu zaidi kuliko wanaume.

“Idadi ya wanawake wanaomiliki simu ni 10.4 milioni na wanaume ni 10.2 milioni,” ikasema ripoti.

Rununu ni mojawapo ya chombo ambacho hutumika sana katika mawasiliano. Miundo ya simu hizi za mkono imekuwa ikibadilika mara kwa mara kadri teknolojia inapoendelea kukua.

Pia, simu hizi zimekuwa vifaa muhimu vya kuendeleza teknolojia kwa kuwa mitandao maarufu kama vile Whatsapp, FaceBook, Twitter na nyinginezo hupatikana kupitia rununu za kisasa.

Pia, ripoti hii ya Sensa ilielezea zaidi kuwa kufikia mwaka wa 2019, kati ya watu wa umri wa miaka mitatu na kuendelea, asilimia 22.6 walitumia intaneti na wengine asilimia 10.4 walitumia kompyuta.

Ripoti pia ilisema kuwa asilimia 4.3 ya Wakenya wa umri wa miaka 15 na zaidi walitafuta na kununua bidhaa na huduma mtandaoni.

You can share this post!

ODM, Chap Chap wataka mageuzi ya mfumo wa utawala

SENSA: Wakenya milioni 7 hawajasoma

adminleo