• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Huu wimbo wa Reggae kamwe haumlengi Ruto – Raila

Huu wimbo wa Reggae kamwe haumlengi Ruto – Raila

Na MARY WANGARI

KIONGOZI wa Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga amefafanua kuhusu wimbo anaopenda wa mtindo wa reggae almaarufu “Nobody Can Stop Reggae” akikanusha madai kwamba unamlenga kisiasa Naibu Rais William Ruto.

Waziri mkuu huyo wa zamani alifafanua kwamba wimbo huo unaoashiria kwamba hakuna anayeweza kwa vyovyote kulemaza juhudi za kufanikisha Mpango wa Maridhiano (BBI), ulikuwepo tangu zamani.

“Huu ni wimbo wa zamani, haukuimbwa jana kuwalenga watu mahsusi. Watu hawa wanaoona mabaya kwa kila jambo, wanajihofia. Wimbo huu haumlengi Dkt William Ruto. Ruto ni miongoni mwa Wakenya milioni 47, hatuwezi kubuni mpango wa kumlenga,” alisema Bw Odinga.

Katika mahojiano na vyombo vya habari, Bw Odinga alieleza kwamba Naibu Rais hapo mbeleni alikuwa amejiunga naye pamoja na Rais Uhuru Kenyatta kupigia debe BBI kabla ya kugeuka na kukosa msimamo.

Huku akifichua kwamba ndiye aliyemnoa kisiasa Dkt Ruto, Bw Raila alionekana kuwa na uhakika kwamba juhudi za naibu rais za kupinga BBI zingeambulia patupu hatimaye.

“Nani angefikiri kwamba Ruto angepinga BBI. Kwanza alikuwa akiiunga mkono kisha akaanza kukosa msimamo thabiti. Sasa anasema anapinga. Anasema atakomesha reggae, tunamtakia kila la kheri,” alisema kiongozi huyo wa ODM.

 

You can share this post!

Tunahitaji mdahalo kung’amua mimba ya mapema...

Coronavirus: Saudia yasitisha safari za Mecca

adminleo