• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:21 PM
Machifu wapewe bunduki – Mbunge

Machifu wapewe bunduki – Mbunge

Na Waweru Wairimu

MBUNGE wa Isiolo Kaskazini Hassan Odha anaitaka serikali kuwapa bunduki machifu wanaohudumu katika kaunti za wafugaji ili wajilinde nazo kando na kupambana na wahalifu.

Mbunge huyo alisema machifu na manaibu wao katika kaunti hizo wanahudumu katika mazingira hatari kutokana na hali kwamba silaha nyingi haramu ziko mikononi mwa wahalifu.

Akirejelea kisa cha wiki jana ambapo wahalifu kutoka Laikipia waliteketeza nyumba ya chifu wa Oldonyiro na nyumba zingine katika eneo la Narasha, Bw Odha alisema afisa huyo wa utawala angezuia uhalifu huo kama angekuwa na amejihami kwa bunduki.

 

You can share this post!

Familia ya mwanahabari aliyeuawa yafika kortini ifidiwe

Wafanyakazi wachafua jiji wakidai malipo ya miezi 3

adminleo