• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 2:56 PM
Kesi ya kuapisha Prof Mugenda yarudishwa kwa Jaji Mativo

Kesi ya kuapisha Prof Mugenda yarudishwa kwa Jaji Mativo

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA Kuu Jumatano ilikataa kuzuia kuapishwa kwa makamishna watatu walioteuliwa na Rais Uhuru Kenyatta kuwa wanachama wa tume ya kuajiri wafanyakazi wa Idara ya Mahakama (JSC).

Badala ya kuongeza muda wa kuzuia kuapishwa kwa Prof Olive Mugenda, Felix Koskei na Patrick Gichohi,  Jaji Wilfrida Okwany aliamuru kesi ipelekwe tena kwa Jaji John Mativo aliyetoa maagizo .

Mnamo Machi 9, Jaji Mativo alisitisha kuapishwa kwa wanachama hao watatu kwa muda wa siku 14.

Mahakama ilisimamisha kuapishwa kwa watatu hao baada ya kuelezwa maoni ya umma kuwahusu hayakuulizwa.

Kituo cha Katiba kiliomba mahakama ifutilie mbali kuchapishwa kwa majina ya watatu hao katika Gazeti rasmi la Serikali.

You can share this post!

Kesi ya Jack & Jill iliyokaa kortini kwa miaka 25...

Korti yadinda kumlazimisha Betty Tett kutambua wazazi wa...

adminleo