• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 7:55 AM
Mifupa ya binadamu iliyopatikana shambani yapelekwa mochari

Mifupa ya binadamu iliyopatikana shambani yapelekwa mochari

Na RICHARD MUNGUTI

MIFUPA ya binadamu iliyookotwa katika shamba moja erneo la Ugunja Ijumaa ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya kaunti ya Siaya na Polisi.

Iliwachukua maafisa wa Polisi siku mbili kuiondoa mifupa hiyo baada ya kufahamishwa na wakazi wa kijiji cha Mundindi.

Iliwabidi wakazi hao kustahimili huku polisi wakiiondoa mifupa hiyo iliyoaminika kuwa ya mwanaume.

Kujikokota huko kwa polisi kufika mahala palipokuwa na mifupa hiyo kuliwakera wanakijiji.

Kulingana na mkazi Bw Antony Odero , mifupa hiyo ilipoonekana karibu na mto Woruoya ikiwa imefunikwa na shati , chifu pamoja na maafisa walienda mahala hapo na kuondoka bila kuchukua hatua.

Shirika la habari nchini KNA lilipozugumza na Afisa mkuu wa Polisi Bw Samuel Koskei kuhusu tukio hilo , alithibitisha kwamba mifupa ya binadamu ilikuwa imeonekana.

Bw Koskei alisema maafisa wa uchunguzi walipelekwa kijijini humo na kuiondoa mifupa hiyo na kuipeleka chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya kaunti ya Siaya.

Uchunguzi umeanzishwa.

You can share this post!

Polisi kukamatwa kutoa ushahidi katika kesi ya ugaidi

‘Wachezaji wa raga waliombaka msanii wakamatwe’

adminleo