• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Gavana Roba na naibu wake watangaza kukatwa asilimia 30 ya mshahara

Gavana Roba na naibu wake watangaza kukatwa asilimia 30 ya mshahara

MANASE OTSIALO NA FAUSTINE NGILA

GAVANA wa Mandera Bw Ali Roba na naibu wake Bw Mohamed Arai wametangaza kuwa watakatwa mshahara kwa asilimia 30 kuanzia mwezi Aprili hadi Juni.

Bw Roba alisema kuwa pesa hizo zitatumika na maafisa wa kupambana na kuenea kwa virusi vya corona.

Kulingana na mkuu huyo wa kaunti, kupunguzwa kwa mishahara kama alivyofanya Rais Uhuru Kenyatta  hapo Jumatano kutasaidia Wakenya pakubwa katika nyakati hizi ngumu za kiuchumi.

“Kusisitiza agizo la rais na wito wa kujitolea kuchangia katika janga hili la corona, mimi na naibu wangu tumejitolea kukatwa asilimia 30 ya mshahara,” gavana huyo alisema mjini Mandera.

Aliongeza kuwa Kamati Simamizi ya Kaunti hiyo ilikutana na kupitisha uamuzi huo, ambapo pia wafanyakazi wa madaraja ya ajira ya T, S na R watakatwa mshahara.

You can share this post!

Mapadre, watawa na waumini 46 wakamatwa kwa kusali kinyume...

Wafungwa 39 waachiliwa kupunguza msongamano magerezani

adminleo