• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 11:59 AM
Kafyu hii iondolewe – LSK

Kafyu hii iondolewe – LSK

By JOSEPH WANGUI

CHAMA cha mawakili nchini (LSK)  kimefika mahakamani kikitaka kuondoloewa kwa kafyu na kumtaka Waziri wa Afya Mutahi Kagwe kutoa taarifa kuhusu jinsi Kenya imejitayarisha kupambana na janga la corona.

Chama hicho kinataka agizo mbadala la kuishurutisha Wizara ya Usalama wa Ndani kuongeza wakati wa kuanza kafyu  kutoka  saa moja usiku hadi saa nne usiku.

Kinaitaka  korti pia kumlazimisha Waziri Fred Matiang’i kuchapisha mwogozo wa jinsi polisi wanapaswa kutekeleza kafyu na kuchapisha kwa gazeti linalosambazwa kote nchini.

Kupitia kwa wanasheria Wakesho Kililo na Omwanza Ombati, chama hicho kinasaka kuundwa kwa kanunuzitakazozuia polisi kutumia nguvu kupita kiasi katika kutekeleza  kafyu na  iwapo polisi watakiuka kanuni hizo basi Inspekta Generali wa polisi Hillary Mutyambai atalaumiwa na kushtakiwa.

LSK kinataka korti kuagiza Bw Mutyambai akome kuingilia vyombo vya habari vinavyoonyesha jinsi kafyu inavyoendelezwa, na taaluma ya unasheria kuongezewa katika orodha ya watoaji huduma muhimu.

IMETAFSIRIWA NA FAUSTINE NGILA

You can share this post!

Wanaougua corona sasa wafika 50, wanabodaboda waonywa

CORONA: Daktari motoni kwa kukataa kuhudumia wagonjwa

adminleo