• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Hakuna chai wala chakula kwa maseneta kikaoni

Hakuna chai wala chakula kwa maseneta kikaoni

NA DAVID MWERE

HUKU maseneta wote 67 wakikongamana Jumanne baada ya Seneti kusitisha vikao vyake hapo Machi 17 kutokana na janga la corona, watalazimika kuandaa kikao bila vitafunio walivyozoea wakati wanajadili masuala muhimu.

Hakutakuwa na vyakuala wala staftahi kama chai kwa viongozi hao. Hata hivyo, maji yatakuwa kwa wingi,

Kama sehemu ya mabadiliko yaliyowekwa huku watu wengi wakiendelea kuugua virusi vya corona nchini, itakuwa lazima kwa maseneta hao kunawa mikono kwanza kabla ya kuingia kwa eneo la mijadala, huku vioefu vikiwekwa kila mahali.

Shughuli ya kwanza itakuwa kusomwa kwa ujumbe kutoka kwa Bunge la Kitaifa kuhusu Mswada wa Ugavi wa Mapato 2020, kisha mswada huo kusomwa kwa mara ya kwanza katika kikao hicho.

 Mswada huo, ambao unatoa taarifa za ugavi wa mapato baina ya serikali kuu na zile za kaunti, ulipitishwa Machi 17 katika Bunge la Kitaifa kisha kupelekwa kwa Seneti ili kupelelezwa.

Mswada huo unatoa Sh2.7 trilioni za matumizi ya taifa huku Sh1.78 trilioni zikitengewa serikali ya kitaifa na Sh316 bilioni zikipewa serikali za kaunti kugawana.

IMETAFSIRIWA NA FAUSTINE NGILA

You can share this post!

Serikali mbioni kusaka waliotangamana na padre wa Kitui

TANZIA: Askofu Mstaafu Ndingi Mwana’a Nzeki afariki

adminleo