• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 5:39 PM
Staa wa Shujaa Allan Makaka afariki

Staa wa Shujaa Allan Makaka afariki

NA AYUMBA AYODI

MWANARAGA aliyekuwa na kasi ya kupindukia Allan Makaka wa timu za raga za taifa ya Shujaaa na Simba ameaga dunia.

Makaka ambaye alikuwa afisa wa mauzo katika kampuni ya Royal Media Services alipata ajali katika barabara kuu ya Mombasa, jijini Nairobi na ofisi za kampuni ya Airtel.

Royal Media Services ilisema kuwa alikuwa mfanyakazi kwa miaka 8 katika chapisho la habari hizo za kusikitisha Jumatano asubuhi kwenye tuvuti ya televisheni ya Citizen.

“Allan alijiunga nasi Februari 1, mwaka wa 2012 kama afisa wa mauzo na baadaye akawa meneja wa biashara katika stesheni ya Hot 96 nafasi aliyohudumu kwa kujitotela.

“Allan amekuwa chombo cha kuwafunza wengine wanaofanya kazi nzuri katika kazi zao. Amekuwa rafiki wa wengi kwenye kampuni.

“Tumekuwa tukishirikiana na familia yake kuomboleza  na tunaomba mtuunge mkono kwa maombi yenu katika wakati huu mgumu,’’ alisema mkurungezi wa RMS Rose Wajohi.

Mchezaji wa zamani wa Ulinzi stars anayehudumu kama kocha msaidizi wa KCB Dennis Mwanja, alimtaja Makaka kwa kumtaja kuwa mwenye nidhamu na maono.

“Tulisoma shule moja ya upili ya Musingu ambapo tulicheza raga pamoja. Nilihitimu mwaka wa 1999 naye Makaka alimaliza mwaka wa 2000 kabla ya kujiunga na Ulinzi,’’ alisema Mwanja, aliyecheza pamoja naye kwenye timu ya Kenya Sevens.

 

Tafsiri: Faustine Ngila

You can share this post!

Viongozi wa jamii ya Kindiki waikemea Jubilee kumvua mamlaka

Uhuru atawaweka hadi 2022?

adminleo