• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Madiwani wa Kirinyaga walifuata sheria kumng’oa Waiguru – Korti

Madiwani wa Kirinyaga walifuata sheria kumng’oa Waiguru – Korti

NA MAUREEN KAKAH

Maakama Kuu imetupilia mbali ombi la Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru la kutaka kutupiliwa mbali kung’atuliwa kwake mamlakani na madiwani wa kaunti hiyo.

Jaji Weldon Korir aliamuru kwamba madiwani wa Kaunti ya Kirinyaga hawakukiuka amri zozote za korti na walifuata sheria kufanya hivyo.

Bi Waiguru alienda kortini kuiomba korti kusimamisha kung’atuliwa kwake mamlakani akidai madiwani hao walikiuka amri ya korti.

Gavana huyo alijijtetea kuwa madiwani hao walikiuka amri ya korti akidai korti ilikuwa tayari imesimamisha kwa muda madiwani hao kujadili kung’atuliwa kwake kwa sababu ya janga la virusi vya corona.

Bi Waiguru alikuwa ameiomba korti itupilie mbali uamuzi huo wa madiwani hao lakini ombi lake likakataliwa. Madiwani 23 kati ya 33 waliunga mkono kutolewa kwa Waiguru kutoka kiti cha ugavana huku suala hilo sasa likielekea katika Bunge la Seneti.

You can share this post!

Polisi 3 waliohusika kumvuta Mercy Cherono kwa pikipiki...

Bajeti yanyonga wanyonge

adminleo