• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Mpango wa kuwarudisha nyumbani Waganda waliokwama ughaibuni wakwama

Mpango wa kuwarudisha nyumbani Waganda waliokwama ughaibuni wakwama

NA DAILY MONITOR

Serikali ya Uganda imeahirisha mpango wa kuwarudisha nyumbani wananchi wake ambao wamekwama nchi za nje, Wizara ya afya ya nchi hiyo imetangaza.

Waziri wa Afya Jane Ruth Aceng alikuwa amesema kwamba watu 300 kati ya 2,392 watakuwa wakirudishwa nyumbani kila wiki na kundi la kwanza linapaswa kufika Jumamosi hii.

Lakini Mamlaka ya Usafiri wa Ndege nchini humo ilisema kwamba haina habari kwamba kuna ndege ya kuleta watu waliokwama nchi za nje.

Baadaye wikendi wizara hiyo ilisema kwamba hakuna ndege itafika humo nchini.

“Huku Waganda zidi ya 2,300 wakirudishwa nyumbani, hakuna ndege inafika nchini kwa sasa. Tarehe halisi itatajwa hapo baadaye.”

Juhudi za kuongea na Wizara ya Afya kuhusiaana na mabadiliko hayo hazikuzaa matunda.

Katibu katika wizara ya afya aliwaelekeza Daily Monitor katika Wizara ya Maswala ya Kigeni.

“Unajua maelezo hayo yana Wizara ya Maswala ya Kigeni, hao ndio wanajua maelezo kuhusiana na usafiri wa wananchi waliokwama nje, kwetu hatuhusiki na usafiri wa ndege,” alisema Dkt Atwine.

Lakini maafisa wa Wizara ya Maswala ya Kigeni hawakupokea simu zetu.

You can share this post!

Magufuli afungua shule na shughuli zilizofungiwa

Ushindi wa 1-0 waipa Bayern kombe la 8 mfululizo

adminleo