• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Wauguzi wagoma kwa mara ya 4 mwaka huu Kisumu

Wauguzi wagoma kwa mara ya 4 mwaka huu Kisumu

ELIZABETH OJINA

Sekta ya afya kaunti ya Kisumu iko mashakani humu mgomo wa wauguzi na maafisa wa afya ukifikia wiki ya mbili.

Mwaka huu pekee maafisa hao wa afya wamefanya mgomo mara nne. Hospitali nyingi za umma zimebakia mahame huku watu wakilazimika kutafuta matibabu kwenye hospitali za kibinafsi.

Mafisa hao walisema hawatarudi kazini mpaka serikali ya kaunti izingatie maafikiano yao ya ajira ya 2017.

Katibu wa muungano wa wauguzi tawi la Kisumu Maurice Opetu alisema kwamba serikali ya kaunti inasema janga la corona ndio sababu ya kutowashughulikia..

Gavana Anyang Nyong’o alisema kwamba serikali ya kaunti si ya kulaumiwa kwa kuchelewa kwa mishahara.

Katika mawasialo na redio katika eneo hilo, gavana huyo alisema kwamba si Kisumu pekee imechelewesha mishaahara bali kaunti zingine zilikuwa zinapitia hayo pia.

Alisema kwamba si maafisa wa afya pekee walioathiriwa kwani wafanyakazi wengine wa kaunti walikuwa wameathirika..

Lakini mwenyekiti wa kamatii ya afya kaunti ya Kisumu Vincent Jagogo aliambia Taifa Leo kwamba kaunti hiyo ilikuwa na chaguo la kuweka mikakati na benki ya kulipa wafanyakzi.

You can share this post!

Wafanyakazi 14 wa Safaricom sasa wana corona

Madiwani wawili wang’olewa kamatini Bunge la Bungoma

adminleo