• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Masharti ya safari za ndege yalegezwa

Masharti ya safari za ndege yalegezwa

Na CHARLES WASONGA

SERIKALI imetangaza kulegeza masharti ya kupambana na virusi vya corona kwa wasafiri wa ndege nchini.

Tofauti na safari za barabarani na treni ambazo itakuwa ni lazima zifanywe kabla saa tatu usiku kafyu inapoanza, Waziri wa Uchukuzi James Macharia jana alisema wasafiri wa ndege watakubaliwa kuwa barabarani hata saa za kafyu.

Kulingana naye, kuna ndege ambazo zitakuwa zikiondoka usiku kwa hivyo serikali iliamua kanuni za kafyu zisitumiwe kwa wasafiri.’

Anayesafiri akipatikana barabarani saa za kafyu, atahitajika kuonyesha polisi tikiti yake ya usafiri na atakubaliwa kuendelea na safari yake,’ Bw Macharia alisema jana.

Kwa upande mwingine, hitaji la watu kukaa umbali wa mita moja pia halitatumiwa kwa safari za ndege.

Waziri alisema hitaji hilo likitumiwa, itamaanisha ndege zitatakikana kubeba asilimia 50 ya wasafiri wa kawaida na hiyo itakuwa hasara kubwa kwa mashirika ya ndege.

Vile vile, wahudumu wa ndege ambao watakuwa wakiingia nchini kutoka nchi za kigeni hawatatakikana kujitenga kutoka kwa jamii kama ilivyo kwa wasafiri.Jana visa vingine 278 vya maambukizi vilitangazwa na kufikisha idadi hadi 8,528.

Akiongea jana katika Kaunti ya Makueni, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alisema wagonjwa 89 walipona, na sasa idadi imefika 2,593.

Waziri Kagwe alithibitisha kuwa wagonjwa wengine wawili wamefariki na kuongeza idadi kufikia 169.

You can share this post!

Masharti makali kwa wanaotaka kwenda mashambani

Majina ya wanakamati bungeni kuidhinishwa Jumanne

adminleo