• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Polisi ashtakiwa kumuua mwenzake

Polisi ashtakiwa kumuua mwenzake

Wyclife Nyandisi Motanya (kulia) ambaye ni afisa wa polisi wa zamani akiwa na kondakta Dengah John Lenda kizimbani Nairobi. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUINGUTI

ALIYEKUWA afisa wa polisi alishtakiwa Alhamisi kwa wizi wa mabavu uliopelekea kuuawa kwa afisa wa polisi.

Wyclife Nyandisi Motanya (afisa wa polisi wa zamani) alishtakiwa pamoja na kondakta wa matatu Dengah John Lenda mbele ya hakimu mwandamizi Bi Martha Mutuku.

Walikanusha mashtaka kumi na mawili ya kuwaibia abiria katika eneo la Baba Ndogo, Ruaraka kaunti ya Nairobi.

Walikana kuwa mnamo Aprili 28, 2018 walimnyang’anya Koplo Martin Korir bastola.

Wakitekeleza wizi huo, washtakiwa yadaiwa walikuwa na bastola na visu.

Walizuiliwa rumande hadi afisa wa urekebishaji tabia awasilishe ripoti kuwahusu ndipo wawasilishe ombi la kuachiliwa kwa dhamana.

Kesi itatajwa Mei 25.

You can share this post!

Walioshukiwa kumuua kondakta kwa kuongeza nauli waponea

Mary Njoroge ateuliwa kusimamia mechi za Kombe la Dunia U-20

adminleo