• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Pasta akana kuvamia shamba Kariobangi

Pasta akana kuvamia shamba Kariobangi

Pasta John Karanja Wanjengu akiwa kizimbani Mei 15, 2018. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

MUHUBIRI wa kanisa la  Kenya Assemblies of God (KAG) alishtakiwa Jumanne kwa kuvamia shamba la wenyewe.

Pasta John Karanja Wanjengu mwenye umri wa miaka 56 alishtakiwa mbele ya hakimu mwandamizi Bi Martha Mutuku.

Alikanusha shtaka dhidi yake na kuomba aachiliwe kwa dhamana.

Pasta Wanjengu alishtakiwa kwa kuvamia ploti nambari 150 mnamo Julai 31, 2006.

Mshtakiwa alikana alivamia shamba hilo akiwa na nia ya kuvuruga amani ya Bw Simon Kuria Wanyoike.

Upande wa mashtaka ulidai Pasta Wanjengu alipania kutwaa umiliki wa ploti hiyo.

Hakimu alimwachilia kwa dhamana ya Sh100,000.

Kesi itasikizwa Juni 18, 2018.

You can share this post!

Jaji Ouko awataka wenzake kujiepusha na ufisadi

Maraga awataka majaji na mahakimu wazingatie maadili ili...

adminleo