• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:45 AM
Achoshwa na dhuluma za kimapenzi, awatilia wazazi sumu

Achoshwa na dhuluma za kimapenzi, awatilia wazazi sumu

Na Stephen Oduor

Mwanamke mmoja na mumewe walihepa kifo Jumamosi baada ya  mwana wao wa kike kuwakwekea sumu kwenye maji ya kunywa nyumbani kwao Bura, Tana River. 

Mshukiwa huyo alichukua sheria mkononi baada ya kugundua kwamba mama yake alishirikiana na babayake wa kambo kwenye kesi aliyowasillisha kwa wazee ya kudhulumiwa kimapenzi.

Kulingana na mjomba wa msichana huyo  msichana huyo alimlaumu baba yake wa kambo kwa kumdhulumu kimapenzi kuanzia akiwa miaka 13 na kumtishia kumuua akidhubutu akisema yaliyotokea.

Mjomba huyo aliambia Taifa Leo kwamba kuna wakati msichana huyo alitoroka na kwenda kuishi na yeye lakini hakumwambia kwanini alikuwa ametoroka kwao.

“Alikuwa anaokenaka myamavu na alikuwa anapenda kujitenga yake wakati mwingine .Hakuwa anataka kuzungumza  wala kuzungumza na binamu wake,”alisema.

Baada ya kuishi na mjombake kwa miezi sita ,mamayake alimuomba arudi nyumbani .

Msichana huyo alisema mama yake alimsaidia kutoa mimba kwenye hospitali ndogo ya Madogo alipogundua kwamba mimba hiyo ilikuwa ya babayake.

Alisema kwamba mama yake alikosana na mwanamume huyo na kuamua kuondoka lakini akarudi tena 2019.

TAFSIRI: FAUSTINE NGILA

You can share this post!

Wawili wafariki kwenye ajali Pwani

Wafaa kunishukuru, Muthama ajibu Kalonzo