• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 9:55 AM
Afa lojing’i akiwa na jamaa

Afa lojing’i akiwa na jamaa

Na MWANDISHI WETU

POLISI jijini Nairobi wanachunguza kisa ambapo mwanamke aliaga dunia baada ya kuugua akiwa katika lojing’i na shemejiye wa kiume.

Mwanamke huyo aliyekuwa na umri wa miaka 42, aliaga dunia punde alipofikishwa katika Hospitali Kuu ya Kenyatta kwa teksi, kutokana na kukohoa na kutapika.

Taarifa za polisi zinasema mama huyo ambaye huishi Mwiki, Kasarani, alifika jijini mwendo wa saa moja unusu usiku kukutana na kaka wa mumewe, aliyekuwa amesafiri kutoka Malindi.

“Walikodisha chumba cha malazi katika hoteli iliyoko barabara ya Dubois siku ya Alhamisi. Asubuhi mwendo wa saa kumi na mbili, mwanamke huyo alianza kukohoa na kutapika,” ikasema taarifa ya polisi.

Shemejiye alichukua teksi na kumkimbiza KNH ili atibiwe, lakini madaktari wakatangaza kuwa alikuwa tayari amekufa.

Polisi walisema wanangojea ripoti ya upasuaji wa maiti kujua kiini cha kifo cha mwanamke huyo.

You can share this post!

Msichana, 12, ndani kwa dai la kumuua mpenziwe

Msiogope kutukosoa, Rais aambia viongozi wa kidini nchini