• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:36 PM
VINYWAJI: Jinsi ya kuandaa ‘smoothie’ ya papai na ndizi

VINYWAJI: Jinsi ya kuandaa ‘smoothie’ ya papai na ndizi

Na DIANA MUTHEU

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 5

Vinavyohitajika

  1. Papai ½
  2. Ndizi 1
  3. Maziwa glasi 1
  4. Blenda
Viungo vinavyohitajika kutengeneza ‘smoothie’ ya papai na ndizi. Picha/ Diana Mutheu

Jinsi ya kuandaa

Toa maganda ya matunda yako kisha yakatekate vipande vidogovidogo ukivitia ndani ya blenda yako.

Ongeza maziwa katika mchanganyo huo wa matunda kisha hakikisha unasaga katika blenda hadi ‘smoothie’ yako ilainike vizuri.

Viungo ndani ya blenda. Picha/ Diana Mutheu

Koroga na umimine katika kikombe chako. Burudika.

You can share this post!

AFYA NA ULIMBWENDE: Ujauzito haumaanishi kupoteza mvuto

Ochan, Sichenje watia saini kandarasi mpya Ingwe huku...