• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Raha kwa wachuuzi baada ya masoko kufunguliwa

Raha kwa wachuuzi baada ya masoko kufunguliwa

NA KEVIN ROTICH

Baada ya shule kufungwa mwezi wa Machi kutokana na mkurupuko was virusi vya Korona, uuzaji wa vyakula, vifaa vya kuandika na pia sare za shule zilitatizwa.

Kutokana na ukosefu wa wanunuzi, wasambazaji walilazimika kuuza bidhaa zao kwa bei ya kutupa ili kuzuia hasara mkubwa.

Lakini agizo la serikali la kufunguliwa kwa shule wiki hii kwa awamu, ni jambo la kufurahisha kwa wachuuzi.

Mmoja wa waliohangaika ni wauzaji wa wa vitabu, kalamu na pensili Merge Sationer katika kaunti ya Kajiado, kaunti ndogo ya Ongata Rongai.

Minica Gathesha anasema uuzaji ulipungua kwa hadi asilimia sufuri kutoka mwezi wa machi.

“Kutoka machi, hatujauza chochote kwani bidha za Januari bado zipo kwenye duka letu,” Bi Gathesha anasema.

Lakini anatarajia ununuzi kupanda kwa asilimia themanini hadi mia moja kuanzia wiki hii wanafunzi wanaporejea shuleni mwao.

“Ni wakati mdogo tu kabla ya hali ya kawaida kurejea,” anasema.

Mwezi wa Oktoba 6, serikali ilitangaza kufunguliwa kwa shule hasa kwenye madarasa ya nne, nane na kidato cha nne kuanzia wiki hii baada ya kufungwa kwa Zaidi ya miezi mitano kutokana na virusi vya korona.

Kulingana na masharti mapya yaliyotelewa na Waziri wa Elimu George Magoha, muhula wa pili utachukua zaidi ya wiki kumi na mmoja.

“Wizara ya elimu inawajulisha ya kuwa kufunguliwa kwa mashule kwa awamu itaanza na darasa la nne, nane na pia kidato cha nane wiki hii,” Profesa Magoha alisema ijuma wiki iliyopita kupitia ujumbe.

Patrick Wanjohi ambaye usambaza mboga katika mashule kwenye eneo la Kasarani mjini Nairobi anasema uuagizaji ulipungua kwa asilimia tisini.

Alikuwa akisambaza zaidi ya kabegi 5, 000 kila mwezi kwa Sh20.

“Ijapo shule zimefunguliwa, bado hatujaponea kwani uharibifu uliofanyika kwenye Uchumi ni mkubwa sana. Biashara itafunguka kidogo lakini bado tunangoea hali itakavyo kuwa,” anasema.

Muhula wa pili utaanza Oktoba 12 hadi Desemba 23 ambapo wanfunzi watrejea majumbani kwa likizo ya krismasi kutoka December 24 hadi Januari 1, 2021 kabla ya kurejealea muhula wa tatu Januari 4 hadi Aprili 16.

Mitihani ya darasa la nane na kidato cha nne vitafanyika Machi mwaka ujao.

Bwana Wanjohi alilazamika kuuza mboga zake katika soko la Githunguri ili kupunguza hasara. Lakini, ilichukua siku tatu kuyauza. “Niliuza kwa Sh10, ambayo ni chini ya asilimia 50 ambayo nilikuwa nikiuza kabla ya virusi vya korona.

“Kwa sasa, nikiuza bidhaa za Sh12, 000 ya kabegi nina furaha,” anasema.

Kwa upande wake, Wangeshi Waithaka ambaye huuza sare za shule katika soko la Uhuru Market katika barabarea ya Jogoo mjini Nairobi anasema ameuza chini ya asilimia kumi kwa ujumla na rejareja kuanzia Machi.

“Kwa wastani, ningeuza zaidi ya sare mia tano lakini kwa sasa nauza chini ya hamsini kwa mwezi,” anasema. Anasema alilazimika kutumia pesa ambazo alikuwa amewekeza katika msimu wa Januari alipopungukiwa na hela.

Niliwatuma sita kati ya waajiri saba wangu kwa kuwa uuagizaji ulishuka. “Lakini, nimewaita watatu wao na wengine nikiwatarajia kurudi siku jumatatu,” anaongeza.

Wanafunzi watakao rudi mashuleni watatarajiwa kuvaa meski, kupimwa joto mwilini na kuzingatia hali ya juu ya usafi. Kutokana na hayo, amejitosa kuunda meski uagizaji ukitarajiwa kupanda wiki hii.

“Kwa sasa natengeneza maski kwa wanfunzi kwa wingi,” anasema. Anasii mashule kupatia tenda biashara ndogo ndogo hasa sare na bidhaa kadhalika za shule.

Nguo zake huuza kutoka Sh130 hadi Sh3, 000.

You can share this post!

Corona inavyoumiza wafugaji wa kuku

Soko la Uhuru linavyowapa riziki wafanyabiashara Nairobi