• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 8:55 AM
IEBC yapiga firimbi ya Nairobi

IEBC yapiga firimbi ya Nairobi

COLLINS OMULO na PIUS MAUNDU

WAKAZI wa Nairobi watapiga kura Februari 18 mwaka ujao kumchagua gavana mpya kufuatia kutimuliwa kwa Mike Sonko.Spika wa Nairobi, Ben Mutura anashikilia cheo cha kaimu gavana.

Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imevipa vyama vya kisiasa vinavyokusudia kushiriki katika uchaguzi huo hadi Desemba 28, kuwasilisha majina ya watu watakaowania mchujo wa vyama husika na pia tarehe ya mchujo.

Baada ya mchujo kampeni zitaanza Januari 18.IEBC ilisema afisa yeyote wa umma anayedhamiria kugombea katika uchaguzi huo mdogo ana siku saba kutoka Desemba 21, 2020 kujiuzulu kutoka ofisi ya umma.

Katika Kaunti ya Machakos, Waziri wa zamani wa Maji, Mutua Katuku jana aliingia katika kinyang’anyiro cha kumrithi seneta wa Machakos, marehemu Boniface Kabaka.

Wengine ni aliyekuwa naibu gavana wa Machakos Bernard Kiala, Musyoka Kala, na mbunge wa zamani wa Kibwezi, Bw Kalembe Ndile.Seneta Kabaka alizikwa Jumanne.

 

You can share this post!

Mwanamke afariki baada ya kutumbukia baharini

Misongamano mijini wananchi wakielekea mashambani kwa...