• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 2:16 PM
Watupa mtoto kwa kukejeliwa kuzaa watoto wengi

Watupa mtoto kwa kukejeliwa kuzaa watoto wengi

Na MASHIRIKA na VALENTINE OBARA

KERALA, INDIA

MWANAMUME na mkewe waliyekamatwa na polisi kwa kutupa mtoto wao walisema walifanya hivyo kwa vile majirani walikuwa wakiwacheka kwa kuwa na watoto wengi.

Bitto Davis, 32, na mke wake Pravitha, 28, walinaswa kwenye kamera za CCTV walikamatwa baada ya mwanamume huyo kunaswa kwenye kamera za CCTV akimbusu mtoto wa siku tatu kisha kumtupa kanisani.

Iliripotiwa kuwa jamaa na marafiki wa wawili hao walikuwa wakiwakejeli wakati Pravitha alipokuwa mjamzito.

“Tayari wana watoto watatu wa kiume wenye umri wa miaka minane, sita na minne na huyu alikuwa ni mtoto wao wa nne,” afisa wa polisi alinukuliwa kusema. Watashtakiwa kwa kutelekeza mtoto na ukatili.

You can share this post!

TAHARIRI: Serikali ijitolee kuzima gonjwa

Mwanamume ashinda Sh120 milioni mara mbili

adminleo