• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 9:55 AM
Jubilee Insurance kuwapa bima Wakenya wa pato la chini

Jubilee Insurance kuwapa bima Wakenya wa pato la chini

Na BERNARDINE MUTANI

Kampuni ya bima ya Jubilee Jumatano ilizindua mpango wa bima kwa watu wa mapato ya chini zaidi nchini.

Kampuni hiyo inashirikiana na kampuni ya Bluewave Microfinance kutekeleza mradi huo.

Huduma hiyo, Imarisha Jamii itapatikana kwa njia ya simu na itafadhili bima ya maisha, ajali ya kibinafsi, ulemavu, na bima ya afya ili kusaidia wananchi wa mapato ya chini kuepuka baadhi ya changamoto maishani.

Watakaochukua huduma hiyo watalipa hata Sh20 kwa wiki na wataweza kunufaika kwa kupata pesa za kufadhili matibabu, mazishi na ulemavu hadi Sh100,000.

Pia wataweza kupokea Sh10,000 pesa za kusimamia matibabu wanapolazwa hospitalini siku tatu au zaidi.

Mkurugenzi Mkuu wa Jubilee Holdings Juliua Kipng’etich alisema huduma hiyo itafanya rahisi kulipa ada ya bima(premium) na upokeaji wa malipo kwa sababu inatumia simu.

Huduma hiyo inatarajiwa kugeuza sekta ya bima nchini kwa sababu inalenga mahitaji ya wateja, alisema Bw Kipng’etich.

You can share this post!

Tenda za serikali sasa kushindaniwa na wananchi

Outering Road iaongoza kwa idadi ya ajali barabarani...

adminleo