• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:03 AM
Watoto 5 wabambwa kwa kubaka msichana kwa zamu

Watoto 5 wabambwa kwa kubaka msichana kwa zamu

Na MASHIRIKA

DEHRADUN, INDIA

WATOTO watano wa kiume walikamatwa na polisi kwa kumbaka msichana mwenye umri wa miaka minane baada ya kutazama filamu za ngono.

Ripoti zinasema wavulana hao wenye umri wa kati ya miaka tisa na 14, walikuwa wametazama filamu hizo kwenye simu ya rununu.

Polisi walinukuliwa kusema kuwa walimhadaa msichana huyo kwenda nyumbani kwa rafiki yao katika eneo la Sahaspur lililo Dehradun, kisha wakamvamia na kumbaka mmoja baada ya mwingine.

Mkuu wa polisi wa Sahaspur, Naresh Rathore, alinukuliwa na vyombo vya habari kusema wavulana hao walifahamu msichana huyo huwa yuko peke yake nyumbani wakati walipomtendea ukatili huo unaoaminika walipanga siki kadhaa awali.

Ilisemekana walimwona mwathiriwa akicheza peke yake nje wakati walipomhadaa aandamane nao.

Wavulana hao waliwekwa kizuizini na kfufunguliwa mashtaka, kisha baadaye wakapelekwa katika kituo cha kurekebisha tabia huku mwathiriwa akitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani.

-Imekusanywa na Valentine Obara

You can share this post!

Kuira bingwa wa Shibetsu Half Marathon

Wanakijiji waua mamba 300 kulipiza kisasi

adminleo