• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
Kibe alishinda kwa njia ya haki – Mahakama

Kibe alishinda kwa njia ya haki – Mahakama

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA ya rufaa Jumanne ilifutilia mbali kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Gatundu kaskazini Bi Anne Wanjiku Kibe.

Majaji watatu walithibitisha ushindi wa Bi Kibe wakisema mlalamishi Bw Clement Waibara hakufafanua katika kesi yake vituo ambako wizi wa kura ulitokea.

Mahakama ilisema kasoro zilizokuwa zinalalamikiwa hazingewezesha mahakama kubatilisha uamuzi wa wapiga kura.

Wakati wa uchaguzi wa Agosti 8, 2017 Bi Kibe alimshinda Bw Waibara na kuimbuka mshindi wa kiti hicho.

Mahakama hiyo ilimlaumu jaji wa mahakama kuu aliyechambua matokeo ya uchaguzi huo ilhali hakuna mlalamishi aliyewasilisha ombi uchunguzi wa kina wa zoezi lote ufanywe.

Jaji Prof Joel Ngugi alifutilia mbali ushindi wa Bi Kibe akisema “ zoezi lilikumbwa na kasoro tele.”

You can share this post!

Saa rasmi za masomo ni 8.00 asubuhi hadi 3.30 alasiri...

Konchellah apoteza kiti chake

adminleo