Habari Mseto

Aliyeahidi kulipa vijana aliohadaa kuwapeleka Afghanistan aambia korti hana hanani

August 24th, 2018 1 min read

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAMKE aliyepatwa na mshtuko kundi la vijana zaidi ya 20 waliposimama kortini na kusema amewatapeli maelfu ya pesa akiwandanganya atawapeleka nchini Afghanistan kufanya kazi huko Alhamisi alieleza mahakama hana pesa za kuwalipa.

Bi Ednah Kendi Kiruki alikuwa ameomba korti mnamo Jumatano apewe muda kufanya mashauri na walalamishi kwa lengo la kuwalipa.

Lakini Alhamisi alipofikishwa kortini tena alimweleza hakimu , “nimeshindwa kupata pesa hizi ninazodaiwa.”

Hakimu aliamuru mshtakiwa arudishwe rumande kusubiri kusikizwa kwa kwa kesi dhidi yake.

Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh200,000 pesa tasilimu ama awasilishe dhamana ya shilingi laki tatu.