• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Jela miaka 10 kwa kuvuruga mfumo wa Kenya Power

Jela miaka 10 kwa kuvuruga mfumo wa Kenya Power

Na BERNARDINE MUTANU

MAHAKAMA moja jijini Mombasa Jumatano iliwahukumu wanaume wawili miaka 10 jela au dhamana ya Sh5 milioni kwa kuharibu mfumo wa Kenya Power eneo la Shimanzi, Mombasa.

Wawili hao Joseph Omuse na Faiz Kazungu, walikubali makosa ya uharibifu huo walipofika mbele ya Hakimu Mkuu Mombasa.

“Wahukumiwa walipatikana na vifaa vya stima Ijumaa wiki jana Agosti 17,” alisema meneja wa usalama wa Kenya Power Geoffrey Kigen.

Kwingineko, Kenya Power ilikamata watu watatu, Moses Khaemba, Dennis Mimo, na Antony Juma katika eneo la Seya, lokesheni ndogo ya Kwanza, Kaunti ya Trans Nzoia kwa kuharibu milingoti ya stima.

Kikosi cha usalama kilipata vyuma vya kupanda milingoti, mshipi wa usalama, msumeno wa nyororo na mlingoti wa mbao.

You can share this post!

Onyo kali kwa wanabodaboda Lamu

BI TAIFA JULAI 25, 2018

adminleo