• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
CMIL-Kenya yatoa mafunzo ya kuboresha uanahabari nchini

CMIL-Kenya yatoa mafunzo ya kuboresha uanahabari nchini

NA FAUSTINE NGILA

Kituo cha Unahabari na Elimu ya Mawasiliano nchini (CMIL-Kenya) kimeshirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (CA) kupitia ufadhili wa UNESCO kuwaelimisha wananahabari, washikadau na asasi za udhibiti wa habari kuhusu mbinu za kuboresha utendakazi katika sekta hiyo.

Mafunzo hayo ya mtandaoni kwa jina ‘Kuimarisha Uwezo wa Washikadau wa Uanahabari na Asasi za Udhibiti kuhusu Elimu ya Mawasiliano’ yalifanyika kwa siku tatu kuanzia Jumanne hadi Alhamisi wiki hii.

Dhamira ya mafunzo hayo ni kuwaelimisha wanahabari wa mashirika mbalimbali pamoja na wataalamu wa mashirika ya serikali yanahohusika na mawasiliano ili kukuza uelewa wa sera za kituo hicho.

Mkurugenzi wa CMIL Kenya executive Jakubu Mwongera aliambia Taifa Leo kuwa mafunzo hayo yatasaidia kutolewa kwa maoni yatakayotumikwa kuboresha mwongozo wa UNESCO kuhusu mtaala wa elimu ya habari nchini.

“Mafunzo hayo yatasaidia pakubwa hasa katika hali ambazo serikali ya Kenya inatekeleza miradi mbalimbali kukuza uelewa wa habari katika enzi hii ya kidijitali kwa wananchi,” alisema.

Kutekelezwa kwa miradi hii kunaweza kuongezea kiwango cha wananchi cha kung’amua jinsi ya kupata habari muhimu zitakazowasaidia kufanya maamuzi ya busara katika maisha yao, hasa kuhusu masuala ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

“CMIL Kenya pia itawalinda wananchi dhidi ya habari feki na kuwawezesha kushiriki katika maendeleo ya kijamii na kisiasa, huku ikiwapa fursa kufaidika na nafasi za ajira zinazotolewa na teknolojia za kisasa,” aliongeza.

Kuinua viwango vya ushindani katika tamaduni mbalimbali huenda kukapiga jeki juhudi za kuwapa maarifa wananchi kupitia vyombo vya habari vinavyofurahia uhuru wa kuchapisha na kutangaza habari, hali ambayo itasaidia kuleta uongozi bora nchini.

 

 

You can share this post!

Lazio wasajili ‘nyani’ mkongwe Pepe Reina

Refarenda ndiyo cheti rasmi cha ‘talaka’ ya...