• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Familia yalilia haki kuhusu mtoto aliyefia shuleni

Familia yalilia haki kuhusu mtoto aliyefia shuleni

Na SAMMY KIMATU

[email protected]

Familia moja kwenye makazi duni ya jiji inataka haki na ukweli juu ya kifo cha mtoto wao katika hali ya kutatanisha wakati wa shule Ijumaa iliyopita.

Benard Mutisya mwenye umri wa miaka sita alidaiwa kugongwa na stima wakati alipokuwa akicheza na watoto wengine katika shule ya Bridge International iliyopo mtaa wa mabanda wa Mukuru- Kwa Njenga, Embakasi Kusini.

Mwalimu wa shule hiyo ambaye alijitambulisha kama kwa jina moja Bi Domiano alisema kijana huyo alikimbizwa katika kliniki ya St Mary Immaculate akapewa huduma ya kwanza na akapelekwa katika Hospitali ya Mama Lucy babake akiwepo.

Alikubali pia katika eneo la tukio, kulikuwa na waya wa umeme ulioning’nia.

Walakini, Bi Winfred Mumbua Kisilu wa miaka 30, mama wa marehemu alikataa madai hayo akisema mumewe, Bw Martin Ndonye Muli wa miaka 30, muashi alikuwa kazini Kiambu.

“Tulitupwa huku na huko wakati tuliuliza juu ya kifo cha mwanangu na tukatumwa kwa polisi huko Embakasi. Je! Inakuwaje mume wangu alishuhudia mtoto akipatiwa msaada wa kwanza katika kliniki ya St Immaculate kwa madai ya mwalimu ilhali alikuwa kazini Kiambu?” Bi Mumbua aliambia Taifa leo.

Nyanyake marehemu, Bi Colleter Mueni mwenye umri wa miaka 45 aliitwa kutoka nyumbani kwake katika kitongoji cha Mukuru-Kaiyaba, hadithi ilikuwa hiyo hiyo.

Anatafuta pia majibu kwa nini wanafamilia waliarifiwa juu ya tukio hilo alfajiri lakini tukio hilo lilitokea mapema asubuhi.

Bi Mueni aliwauliza viongozi waangalie kwa undani suala hilo na waseme hadharani kilichomuua mjukuu wake.

“Tulihakikishiwa na polisi kwamba ni matokeo ya upasuaji wa mwili na daktari wa serikali tu yataonesha kile kilichomuua kijana,” Bi Colleter akasema jana.

  • Tags

You can share this post!

Watu 6 waangamia katika ajali ya Mazeras

Poghisio amkejeli Lonyangapuo kubadilisha mawaziri kila mara

adminleo