• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Wanasiasa wataka Jubilee iwe macho Raila asije akazima ndoto ya Ruto 2022

Wanasiasa wataka Jubilee iwe macho Raila asije akazima ndoto ya Ruto 2022

GAVANA wa Kiambu Bw Ferdinand Waititu. Picha/ Maktaba

Na LEONARD ONYANGO

BAADHI ya wanasiasa wa Jubilee sasa wamesema kuwa hawamwamini kinara wa NASA Raila Odinga kwani huenda akavuruga mpango wa Naibu Rais William Ruto kuwa rais 2022.

Wakiongozwa na Gavana wa Kiambu, Ferdinand Waititu ‘Babayao’, mbunge wa Kikuyu Kimani Ichungwa na Mwakilishi Mwanamke wa Nyeri Rahab Mukami, wanasiasa hao walisema japo wamefurahishwa na hatua ya Rais Uhuru Kenyatta na Bw Odinga kukubali kufanya kazi pamoja, kuna haja kwa Jubilee kuwa waangalifu.

“Tumefurahishwa na viongozi hao wawili kukubali kufanya kazi pamoja lakini Bw Odinga haaminiki,” akasema Bw Waititu.

“Naibu wa Rais, Bw Raila akikuambia ufumbe macho muombe usifunge macho kwani anaweza kutoweka na kukimbia na kila kitu,” akasema Bw Waititu. Bw Ichungwa alimtaka Bw Odinga kuwa mwaminifu na asiwe na ‘mguu mmoja nje’.

Bi Mukami alimtaka Bw Odinga kushirikisha vigogo wenzake wa Nasa katika meza ya mazungumzo na Rais Kenyatta ikiwa kweli ana nia ya kuunganisha Wakenya wote.

Lakini Bw Ruto ambaye alikuwepo wakati wa ibada katika kanisa la PCEA mtaani Runda, Nairobi alikwepa na madai ya viongozi hao huku akisema kuwa ushirikiano baina ya Rais Kenyatta na Bw Odinga unalenga kuleta amani ambayo ni muhimu kwa maendeleo.

“Ushirikiano wa Rais Kenyatta na Bw Odinga si wa manufaa ya kibinafsi bali ni wa kuhakikisha Kenya inapata amani hivyo kupisha maendeleo,” akasema Bw Ruto.

You can share this post!

Uingereza yawapa onyo raia wake kuhusu shambulio la kigaidi...

Jumapili ya Mitende ilivyoadhimishwa nchini

adminleo