Habari

Baba aua watoto wake 2 kwa kuwapa yoghurt yenye sumu, na kisha kujinyonga

Na DAVID MUCHUI April 16th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

WATOTO wawili, Rayvan Baraka, 8, na dadake Nova Jay, 3, walikuwa wakicheza nyumbani kwao eneo la Muthara, Kaunti baba yao, David Mwenda, 32, alipowasili nyumbani.

Mwenda, mwanabodaboda, alikuwa ametengana na mkewe kufuatia migogoro ya ndoa na kurudi kwa wazazi wake.

Baba huyo aliwaletea watoto wake maziwa ambayo walikunywa bila kujua yalikuwa yamechanganywa na sumu.

Baadaye, wakazi walipata mwili wa Mwenda ukining’inia ndani ya nyumba, huku watoto hao wawili wakiwa wamezimia na majeraha kichwani.

Watoto hao walifariki dunia wakiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Meru Level Five.

Chifu wa eneo la Thubuku Bartholomew Mwika, alisema inasadikiwa Mwenda aliwalisha watoto sumu kisha akawapiga kabla ya kujiua.

Uchunguzi unaendelea kubaini sababu ya tukio hilo. Mwenda alikuwa amevunjika mguu Oktoba mwaka jana, hali iliyomfanya kushindwa kukidhi mahitaji ya familia yake.

Ndugu yake, Paul Mwongela, alisema ajali hiyo ilichochea matatizo ya ndoa.

Familia sasa inahangaika kukusanya Sh400,000 kugharamia mazishi na matibabu. Wadau wameonya kuhusu ongezeko la visa vya ukatili wa nyumbani kaunti hiyo.