Habari

Benki ya Dunia yapendekeza avokado itozwe ushuru wa VAT

Na VINCENT OWINO NA DOMINIC OMOND June 1st, 2025 Kusoma ni dakika: 1

BENKI ya Dunia inapendekeza Kenya itekeleze ushuru wa ongezeko la thamani (VAT) wa asilimia 16 kwa bidhaa za msingi kama nyama, unga wa ngano, avokado, kahawa, na dawa za meno. Ikiidhinishwa, hatua hii itasaidia serikali kukusanya mapato ya Sh78.4 bilioni zaidi.

Kwa sasa, bidhaa hizi ziko kwenye orodha ya msamaha wa VAT, hali inayowezesha wauzaji kutowatoza wateja ushuru huu. Hii husaidia kupunguza gharama kwa watumiaji wa kipato cha chini, hasa kwenye bidhaa za chakula.

Hata hivyo, Benki ya Dunia inadai kuwa bidhaa hizi si muhimu sana kwa familia maskini na zinachukuliwa kama “anasa.” Miongoni mwa bidhaa zingine zinazopendekezwa kuondolewa kwenye msamaha wa VAT ni vitafunwa na ada za huduma za posta.

Benki hiyo inaamini kuwa mabadiliko haya yataongeza mapato na kusaidia kupunguza umaskini na ukosefu wa usawa nchini Kenya.