Kimataifa

Uganda sasa yatangaza kutokomeza kabisa Ebola nchini mwao

Na REUTERS July 28th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KAMPALA, Uganda:

WAZIRI wa Afya wa Uganda, Chris Baryomunsi, ametangaza rasmi kuwa nchi hiyo haina maambukizi ya Ebola baada ya kudhibiti msambao wa hivi punde uliowaambukiza watu 20 na kusababisha vifo vya watu wawili.

Mkurupuko huo uliotangazwa katikati ya Mei ulihusisha pia watu 15 waliopata maambukizi katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ambayo ndiyo kitovu cha ugonjwa huo.

DR Congo imeendelea kusajili zaidi ya visa 3,000 vilivyothibitishwa vya Ebola.

Baryomunsi alisema Wizara ya Afya ilifuatilia ugonjwa huo kote nchini tangu mkurupuko ulipoanza na ikashawishiwa kuwa sasa maradhi hayo hayapo.

“Katika kipindi chote hicho, wizara iliendelea na kutathmini hali nchini kote na hakuna kisa kipya cha Ebola kilichogunduliwa,” akasema.

Tangazo hilo ni afueni kwa Uganda baada ya juhudi za muda mrefu za kudhibiti maambukizi na kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo hatari katika eneo la Afrika Mashariki.