Korti yakataa ombi la wakili la kutokamatwa kwa tuhuma za kupokea pesa za kuhonga jaji
MAHAKAMA Kuu Jumatatu, Aprili 20, 2026 ilikataa ombi la wakili jijini Nairobi, Kimani Wachira, la kuitaka itoe amri ya dharura ili asikamatwe kwa tuhuma za kupokea Sh1 milioni ili kumhonga jaji.
Jaji Roseline Aburili alisema Wachira hakutoa hoja nzito kwa nini ombi lake lishughulikiwe kama la dharura.
Bi Aburili alisema wakili huyo tayari alikuwa ameachiliwa kwa dhamana ya Sh200,000 na Tume ya Maadili ya Kupambana na Ufisadi (EACC) na hakukuwa na ushahidi kuwa kuna kesi nyingine ya uhalifu dhidi yake.
Badala ya kuridhia ombi lake, Mahakama ilimwaamrisha Wachira awasilishe nakala ya kesi kwa EACC, Mwanasheria Mkuu, aliyekuwa Waziri Raphael Tuju na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma.
Wachira alielekea kortini mnamo Machi akishutumu mashirika ya serikali akidai yalikuwa yakipanga kuwasilisha mashtaka ya utoaji hongo dhidi yake.