Bambika

Matonya ahangaika kupata dhamana ya nusu milioni katika kesi ya ubakaji

Na SINDA MATIKO April 28th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MSANII wa Tanzania, Matonya, amekuwa akihangaika kupata dhamana ya Sh500,000 aliyowekewa na mahakama ya Mombasa baada ya kushtakiwa kwa kosa la ubakaji yapata wiki mbili zilizopita.

Kwa mujibu wa rapa mkongwe kutoka Pwani Kaa La Moto, kumepatikana mshikaji wa Matonya aliye Mkenya ambaye ameamua kumwekea dhamana hiyo.

“Kuna mshikaji ambaye ametoa gari lake kumsimamia Matonya kama dhamana, maana masharti ya mahakama ni kwamba lazima iwe Mkenya. Mchakato huo ndio tumekuwa tukiendelea nao,” Kaa La Moto alifichua.

Matonya alitiwa kizimbani kwa madai ya kutekeleza kitendo hicho cha unyama kwenye mjengo mmoja mtaani Nyali.

Ni mashtaka aliyokana  msanii huy wa Bongo na akapewa dhamana ambayo amekuwa akisakasaka kuipata ili aweze kufanya kesi hiyo akiwa nje.

Aidha, korti ilimwamuru kuwasilisha  pasipoti  yake.