Bambika

Ndugu zangu walichangia ndoa yangu kuvunjia, mcheshi Wilbroda afunguka

Na SINDA MATIKO October 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MCHEKESHAJI Jacque Nyaminde alaamurufu Wilbroda, kawatemea povu ndugu na jamaa zake kwa kumvunjia ndoa.

Mwigizaji huyo wa zamani wa Papa Shirandula anakiri kuwa ndugu zake walichangia pakubwa kuvunjika kwa ndoa yake, jambo analosema alikuja kugundua baadaye.

“Nami pia nilichangia kuvunjika kwa ndoa yangu na nafikiri ni kwa sababu niliwaruhusu jamaa zangu kuishi na sisi. Nilikuwa nao muda wote, dada zangu siku zote walikuwa nyumbani kwangu. Ushawishi wao ulichangia na nilikuja kugundua baadaye sababu kipindi kile sikuona kama ni tatizo.”

Tangu ndoa yake ivunjike zaidi ya miaka mitano iliyopita, Nyaminde aliwapiga marufuku jamaa zake nyumbani kwake. Siku hizi ni lazima mtu amtaarifu kabla ya kumtembelea.